Zilipendwa


Comments

170 Responses to “Zilipendwa”

  1. sungael michael on January 3rd, 2008 2:00 am

    kwa muda mchache niliotumia kusikiliza nimeona kazi yenu ni safi sana. Pia kwa haraka nimegundua kasoro moja wimbo wa “sina ndugu” ulicharazwa na maquis du zaire sio marijani rajab kama inavyosomeka katika orodha ya nyimbo zenu. mengine yakiwepo sitasita kuwajulisha. asanteni sana kwa hii zawadi ya new year.

  2. Deo Mugoa on January 3rd, 2008 6:06 am

    Good job done.like us old timer we do need this type of tune/hits to remid us our good old days.
    so how can i get the CD of zilipenwa
    I am in Toronto,Canada

    Also i would like to have Novelle Generation by Lipua Lipua plus Kamiki Yeye

  3. jane on January 3rd, 2008 7:42 am

    I like this web

  4. jane on January 3rd, 2008 7:45 am

    Oliver N’goma Nyimbo zangu tamu kweli kweli uko fit

  5. jane on January 3rd, 2008 11:29 am

    Nime furahi kuona kuwa mtukumbuka hata sisi wazee wa zamani kwa kutuanzishia blog hii ambayo tunaweza kupata kitu ile roho inapende. kazeni but

  6. khalid mohammed on January 3rd, 2008 11:50 am

    hi to all!!!!!!!!!!!!!

  7. Ron on January 3rd, 2008 12:50 pm

    Thank you Jambonet for this wonderful collection!
    Miziki hii inanikumbusha mbali sana. Ninapoisikiliza hukumbuka mambo
    mengi, sehemu nyingi nilizowahi kuishi na watu wengi niliokutana nao ambao kwa pamoja tuliisikiliza, kuifurahia na tuliicheza. Asante sana!

    Je ninaweza kuinunua hii collection kama ilivyo au kuchagua baadhi ya nyimbo.
    Tafadhali nijulishe kupitia anuani hiyo hapo juu.

    Asante sana.

  8. steven kimaro on January 3rd, 2008 1:53 pm

    Ee Bwana sio mchezo nafagilia sana hii blog,tunapata burudani safi,japokuwa sikuwepo enzi hizo itakuwa poa kama mkiweka na bongo flava pia.

  9. zeby on January 3rd, 2008 1:55 pm

    napenda hii collection je naweza kuinunua kama ilivyo. tafadhali naomba kujulishwa.

  10. Matulanya on January 3rd, 2008 1:59 pm

    mdau nakupa hongera zangu za uvunguni mwa moyo wangu kwa kuweka site hii ya oldies..hao vijana wa les wanyika wananikosha sana roho niwasikilizapo…keep it up man..nimeipenda kazi yenu

    wabeja sana

  11. xuma on January 3rd, 2008 2:27 pm

    Mungu awabarikini jambo network. Niko RTP North Carolina na nilikuwa mpenzi mkubwa wa most of these songs especially kutukumbusha utoto/maisha yetu na kuturudisha karibu zaidi na nyumbani. Keep up with a good job

  12. NAKUHAJA on January 3rd, 2008 2:44 pm

    NIMEWAZIMIKIA KISHENZI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! KEEP IT UP.

  13. AVELIN on January 3rd, 2008 2:48 pm

    NIMEFURAHI SANA KWA KUSIKILIZA ZUKU HIZI ZA MONICA SEKA…………..YAANI ZIMENTACHI ILE MBAYA MPAKA NIMESHINDWA KUFANYA KAZI, SIJUI NTAMUELEZA NINI BOSI WANGU, BWANA MICHUZI UNATISHA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

  14. Gilbert on January 3rd, 2008 3:15 pm

    I must say this web remind me of those good days! Keep it up guys.

  15. Paul Nyingo on January 3rd, 2008 5:40 pm

    AAAAAAAAAAAAAAAAAAAA HII MFUENI YA LIPUALIPUA IMENIKUMBUSHA FAR KINOMA KAZENI BUTI WAZEE

  16. Gallus on January 3rd, 2008 6:18 pm

    ah jamani kuna siku huwa zinaganda, sasa kwa mtindo huu wa hizi zilipendwa jamani nadhani nimepata kitu muafaka kufanya siku iwe njema huu wimbo wa franco Nabari misele umenikumbusha miaka ya 1980,1981,82, 83 kule Sumbawanga, my father alikuwa na hiyo kanda kweli mmenikumbusha mbali mno BIG up sana, natumai mngeweza kuuza hizo collections mwaweza kuwa ma MIlionea,

  17. Deo on January 3rd, 2008 6:51 pm

    Mambo murua
    Baada ya kusikiliza baadhi ya nyimbo, kweli mumefanya kazi kubwa asilimia kubwa imegusa miziki yote iliyopendwa na inayoendelea kupenwa.
    Hongera sana kwa kulendeleza Libeneke.
    Bado tunalakujivunia wakati wetu ulikuwa babu kubwa,hivyo Kizazi kipya hakitubabaishi.
    Keep up the good work. And please don’t shut or close down the website.
    We do need This Website to keep our spirit alive and high.

  18. Upendo Furaha on January 3rd, 2008 7:18 pm

    Naipenda sana blog hii. “Big up”

  19. www.yahoo.com on January 3rd, 2008 8:06 pm

    hamna shida mimi nitakufa na wengi

  20. www.yahoo.com on January 3rd, 2008 8:07 pm

    usijali

  21. Mfumu on January 3rd, 2008 8:16 pm

    Ubunifu wenu unastahili kupongezwa, binafsi nimeburudika na kukumbuka miaka ya 78, wakati nikiwa nasikiliza sana radio Bujumbura, jioni.
    Ombi langu kama mtaweza, tafuteni nyimbo za mzee john ondoro chacha(kwa sasa nadha yuko Dar kule shekilango)zinapatikana KBC, na zile za Frenk Humblicks na dada zake, kama wimbo wa vipembe. Vinginevyo ninawaheshimu kwa utundu wenye kuleta furaha mioyoni.

  22. Julius Katanga on January 3rd, 2008 8:44 pm

    This is owesome.
    Most of listeners will agree with me when I call this website ‘off the hook’.It drives me all the way back in days where we used to shake our junk and trunk.I,personally, appreaciate the good job you guys are doing.I currently reside in DC but when I listen the old skool through this web and watching TVT,Star TV and chanel 10 through jump TV, I down deep feel my sweet home Tanzania.Thank you Michuzi and whoever enginered to do this mgnifficent job of putting this polluted planet into our finger prints.
    Congratulations.

  23. Concord on January 3rd, 2008 9:05 pm

    Mambo mazito haya….inanirusisha miaka ileeee Jeans za Michael Jackson,Shati zajuliana,kung fu shoes na za ujiuji…
    KEEP IT UP…..

  24. Lazaro on January 3rd, 2008 9:35 pm

    Asanteni kwa nyimbo zilizopendwa, niusikiapo wimbo wa sisili na masasu nakumbuka nilipokuwa mdogo naishi Keko machungwa.
    Yaani natamani kulia kwani mtu unatamani maisha yale ya muda huo yarudi tena, kitu ambacho hakiwezekani.

    Pia nawakumbuka wale wote walitutoka na ambao nilifurahi nao wakati huo. ndugu na jamaa pia.

    Mola awazidishie na kazi yenu nzuri.

    Genuine Guy- Lazaro. as known as Rico-Star.

  25. Born 2 Suffer on January 3rd, 2008 9:37 pm

    Site bombaa sana hii nyimbo zinanikumbusha mbali saaana yani keep it up.

  26. Born 2 Suffer on January 3rd, 2008 9:40 pm

    Yani hutamani kuondoka katika Computer

  27. MICKEY JONES - COPENHAGEN DENMARK on January 3rd, 2008 11:01 pm

    Ukumbusho mzuri wa enzi hizo za ujana wetu……kazi mzuri mliyoifanya ya kutupa burudani za mwaka mpya 2008!!!

  28. Miss Hoffm.. on January 3rd, 2008 11:04 pm

    Hi guysssss mmenifurahisha sana tena sana nakumbuka mabao mengi na mambo mengi , oooh sijui niseme nini… God blees u… ever
    Sasa tukitaka hizi collection tutapata vipi? Happy new year

  29. Chichi on January 3rd, 2008 11:08 pm

    Its absolutely the bomb!!! Thank you guys for taking me back to the good old days!!
    :o)

  30. MICKEY JONES - COPENHAGEN DENMARK on January 3rd, 2008 11:33 pm

    Zilipendwa zimetupa “GET IT TOGETHER” ya furaha hadi hivi sasa bado tupo katika sherehe ya kukumbuka enzi hizo za zamani tukiwa huko nyumbani - Bongo…tunaendelea mpaka usiku …ingawaje wamekosekana Mbaraka Mwinshehe, Patrick Balyisidya wa AFRO- 70 na Shabani Marijani kuongezea furaha ya zilizopendwa…tumefurahishwa na hii kazi yenu kwa sasa.

    BADO TUNAENDELEA TUTAKUAGENI TUKITOWEKA……..

  31. Tuma Dandi on January 3rd, 2008 11:43 pm

    nawapongeza timu yote iliyoshiriki kufanikia sisi wazee wa sasa na vijana wa zamani kupata nyimbo hizi. nauliza swali, je twawezaje kuzipata nyimbo hizi kwenye cd?

    mwisho kabisa, kuna baadhi ya nyimbo title zake siyo za kweli na waimbaji wake, nafikiri ni kasoro ndogo mnazoweza kurekebisha, vinginevyo nawapa shavu!

    Dandi-UDSM

  32. Christine on January 3rd, 2008 11:59 pm

    Kwa kweli nawafagilia sana blog hii kwani wananikumbusha mbali sana ,japo kumekuwapo na kusitasita au kukwama kwama kwa nyimbo laki ni bomba sana.Ningefurahi sana iwapo ningepata CD za nyimbo zote za zilipendwa kama ilivyo kaktika orodha yenu.

  33. Robert Eli on January 4th, 2008 1:28 am

    Nyimbo nzuri na zimetulia kwa kweli zinatoa liwadha yakikweli kweli na nadhani ni dedication pia kwa wenzetu wanaoteseka Kenya kwa sasa. Tujulishe tutapataje CD au tupe offer ya kuzidownload,kazi njema,keep it up! Hali kadhalika zinaelekeza jamii yetu kuthamini miziki yetu ya asili ya Kiafrika maana sio ya kishenzi as baadhi ya wadau wanavyodai!

  34. steven kimaro on January 4th, 2008 2:06 am

    Aisee nawafagilia sana kwa kazi nzuri mnazofanya.,yaani mimi sasahivi kila napotoka shule ni lazima nijiburudishe na zilipendwa,naomba kama tunaweza kupata CD itakuwa poa sana,watanzania wengi hapa luton uingereza wanazungumzia zilipendwa,aksante sana.

  35. Frank Kambira on January 4th, 2008 2:27 am

    Nimekubali! hii mwisho… yaani napata “Kasongo yeyeee…” Super Mazembe hao… Na huku Mbaraka anakwambia nimehamia Mtaa wa 7! Shekhe nashukuru saana kwa hii site - please keep it up… more musik

  36. Ganje on January 4th, 2008 3:41 am

    This is great guys you are fantastic i would like to thank you so much for reminding me the good old days, so keep it up i know its early stages, however i would like you guys to stick to strictly African not Phil Collins and Elton John on this list next time when you edit please add artist such as jb mpiana and werrasson or wenge bcbg and zaiko. thank you very much

  37. sinda on January 4th, 2008 5:51 am

    hey shukurani to everyone who has a hand on this, it brings memories. sasa keep it up kazi nzuri. kaza buti!

    thank you

  38. Hery on January 4th, 2008 6:02 am

    Nimeipata leo jioni hii website. Sijapata muda mzuri wa kusikiliza nyimbo za kunitosha. Nitaendelea nayo jumapili. But it seems like this is what i was looking and waiting for. Babu kubwa wadau wa hii website kwa kutukumbusha zamani sana ndani ya Bongo.
    Hery in Connecticut, US

  39. tefya on January 4th, 2008 6:07 am

    Thanks ,I am enjoying your work.

  40. jane on January 4th, 2008 7:42 am

    Nimefurahishwa na Collection zenu hizo za zilipendewa Ninataka kuzisilikiliza nitafanyaje ili niwe nasizisikiliza kupitia blog yenu hii hii. Naomba Nitumie kupitia E-mail yangu ili niweze kuburudika.

  41. Cloud on January 4th, 2008 7:52 am

    Yaani ninyi ni funika bovu, sijui hata cha kuandika maana mmenikumbusha mbali ile mbaya na moyoni kupata burudani.
    Wakati mwingine najikuta ninacheza au kuimba hizi nyimbo na niko kibaruani, acha tu. Sasa inakuaje maana kuna amethubutu kuniambia nimuwekee kwende CD nyimbo hizi zilipomkuna nikamueleza haiwezekani yeye ananiambia nifanye jitihada zote hahahahahaaaa inakuaje bhagosha. Na hatoki hapa kwenye computer yangu yeye anataka nyimbo tu.

  42. agnes on January 4th, 2008 9:34 am

    mm mbona siwapati???najaribu lkn sisikii nyimbo zenu

  43. betty on January 4th, 2008 11:09 am

    Well done, thanks you so much.

  44. Jane on January 4th, 2008 1:07 pm

    Jamani mie nazipata ila zinakwamakwama sana, sizipati straight, natamani ziimbe moja kwa moja, nifanyeje? au ni udhaifu wa komputa yangu? nisaidieni mzee mwenzenu niachana na haya masebene ya watoto wa ubongo wa fleva!!

  45. joshua on January 4th, 2008 2:11 pm

    Nimefurahishwa na hizi zilipendwa yaani wewe acha tu zinanikumbusha enzi za miaka ya themathini nikiwa bado mdogo.

  46. Cathy on January 4th, 2008 2:29 pm

    Thankx Michuzi, ila duh nyimbo ukisubiri iimbe inaaanza kwa bits fresh ila inakata kata sana hebu fanya makalavee mambo yawe smoooooth!! ila hongera sana

  47. mfullah on January 4th, 2008 2:39 pm

    kweli nimefurahi, nime-enjoy maana inanikumbusha mbali sana kwani wengine tumekwisha kua wazee,
    so kee it up guys

  48. joshua on January 4th, 2008 3:17 pm

    Mungu wape ufahamu wa kutupatia miziki ya zamani kwani niukumbusho kwetu sisi vijana wa zamani.

  49. aloyce on January 4th, 2008 3:32 pm

    Miziki hii inankumbusha miaka ya themanini enzi nikiwa naanza shule ya msingi kwaujumla ni miziki mzuri sana asante

  50. Gilbert on January 4th, 2008 4:31 pm

    Like Zeby asked, is it possible to buy collection this collection from you? Waiting for your reply.

  51. kweba on January 4th, 2008 5:22 pm

    kheri ya mwaka mpya jambonetwork! hongereni kwa kazi hii nzuri kuturudishia ‘an alternative’ katika burudani hii ya muziki!! napenda kusahihisha kidogo hapo kwenye playlist yenu: wimbo ‘africa liberte’ uliimbwa na franklin boukaka toka congo na siyo dibango, wimbo ‘misile’ naona???? huu umeimbwa na tp ok jazz chini ya freddy mayaula mayoni. hongereni saana !

  52. mike on January 4th, 2008 5:46 pm

    oohn mdau hii miziki unaweza kushiba bila kula enzi hizo hata ndege walikuwa wanaimba ,siku hizi ni kunguru tu.hongera sana kwa mpangilio wako mzuri wa the old school.

  53. Dennis Mwendwa on January 4th, 2008 6:12 pm

    kwa kweli jambonet nawapongeza sana kaw kazi nzuri na mkusanyo mzuri wa nyimbo za zamani ili hata sie tulio huku ughaibuni tuweze kukumbuka enzi zetu huko nyumbani.
    hii ni zawadi nzuri sana kwa mwaka huu, naomba kama mtaweza pia wekeni wimbo wa “homa imenizidia”

    pongezi nyingi toka uingereza!!!!

    kheri ya mwaka mpya kwa watumiaji wote wa globu hii!

  54. mtilila yassin on January 4th, 2008 7:26 pm

    Hii web ni babu kubwa,kwakweli naikubali kazi yenu kwani inatufanya tukumbuke mambo mazuri ya zamani,binafsi vibao kama Maze na Ibeba vya Tabulei na Boreau deq bonyenye–Madilu Coeurs!! aaaaa we acha tu,yaani vinanikumbusha enzi za Disco.

  55. jaki on January 4th, 2008 11:55 pm

    Mdau weye kiboko, nimeacha kufanya assignment natakiwa nisubmit kesho morning, nala tu mziki wa zilipendwa, umenikumbusha utotoni mzee.

    Keep it up!

  56. Zablon on January 5th, 2008 1:39 am

    Hey! Ilove this collection! I mean it is awsome, wonderful and I enjoy every minute I listen to it. I just missed one song JULIA of KOFI OLOMIDE, can somebody get it from somewhere! I can buy the collection just let me know how! Congratulation to Jambo Forum!! Asante sana

  57. Rizy on January 5th, 2008 3:29 am

    nyimbo zimenifurahisha sanaaaaaaaaaaaa………zanikumbusha mbali hadi zataka kuniliza………………….kazi nzuri sana………….safiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!!

  58. william on January 5th, 2008 3:33 am

    Jamani tunaomba kuchangia nasi kwa kazi yenu hiyo nzuri kwa kununua CD zenu,hivyo tujulishabe ni namna gani tunaweza pata hizo collection.

  59. Festo Damian on January 5th, 2008 4:52 am

    Ahsante kwa kunitumia huu mtandao. Kwa kweli mambo naona ni poa kwani nyimbo hizi zimenirudisha home kabisa !!!

    Festo

  60. mwita chacha on January 5th, 2008 2:49 pm

    Going back to those years where audio cassette were not fond in TZ ,most yof these song were availlable on Disic plate( santuri).You guys you are bringing back my childhood ! Good job, keep it up.

  61. kweba on January 5th, 2008 5:55 pm

    hongereni sana wana jambonetwork kwa kutupa nafasi ya kukumbuka tulikotoka.naomba kutoa masahihisho kidogo hapo kwenye playlist: wimbo ‘africa liberte’ uliimbwa na franklin boukaka toka congo brazza; na wimbo ‘misile’ ni wa tp ok jazz chini ya mayaula mayoni.

  62. Dj. PM on January 5th, 2008 9:38 pm

    Ebwana si mchezo!!!! inabidi mtafute means za kuuza hizi nyimbo, keep it up!

  63. Matulanya on January 5th, 2008 11:33 pm

    Mdau Tuwekee nyimbo za wana TOMATOMA kama nyimbo zi[po kwenye library yako.Baadhi ya nyimbo zao zilizovuruga watu akili enzi hizo ni kama ….nachelewa Stendi ya basi na laiti moyo ungekuwa na kifuniko…. Ingawa bendi hii haikudumu sana kwenye ulimwengu wa muziki wa dance ila ilitoa vitu vizuri vilivyopendwa…km vipo itapendeza mkivijazia humu tujikumbushe enzi hizo

  64. Joyce on January 6th, 2008 4:03 am

    Oh wow…nilitaka kulia wimbo wa sikinde “Ubaya uliuanza zamani…” jamani nilikua std 2 huu wimbo ulikua unachaguliwa na wafanyakazi wengi tu katika kipindi chao cha wafanyakazi… Kikianza tu basi nakurupushwa kaoge shule karibuni…….Nilikua naenda shule saa sita na nusu

    Those were the days….. I miss so much those days……

    I hope watoto wetu wa kizazi hiki nao wakikua watakumbuka good times na wazazi….mhhhh I doubt watakumbuka mananny, baysitter, playstation, ipod and myspace…

  65. Datch Mkally on January 6th, 2008 6:11 am

    Yaani maendeleo ni pamoja na kuchukua yale bora ya zamani. hivi vitu kwa sasa ni agharabu kuvipata na wala havipatikani TENA . unanirudisha nyuuma kiasi nashindwa kupata maneno mazuri ya kusema lakini hii web kwa sisi vijana wa TANU NA ASP ni machozi tu unaposikiliza hizi nyimbo. KAZA BUTI MICHUZI UNANIKUMBUSHA ENZI YA SAFARI RESORT bado ukiwa mvulana. ENDELEA KAZI NI NZURI , TUKO WENGI NYUMA YAKO

  66. Datch Mkally on January 6th, 2008 6:15 am

    Samahani MICHUZI , huo wimbo wa AFRICA LIBERTE kwa kumbukumbu zangu haukuchezwa na MANU DIBANGO ila huo wimbo umechezwa na FRANKA BOKAKA fanya marekebisho NAIKUBALI KAZI YAKO

  67. Paul Nyingo on January 6th, 2008 6:33 am

    jamani jambo mtatuuwa kwa kufikiria enzi zetu yaani hawa shikashika wananikumbusha pale Ifakara sekondari -IFOZA-MACHIPI kwenye madisco ya sherehe za mabweni miembeni nk NGONGI AMON NGONGI ,SEZALI YULIAN etc mnazisikia hizooooooooooooo hii ni ile miaka ya 1979-1983

  68. jo lipaki on January 6th, 2008 7:34 am

    hongera sana ila ningependa nyimbo ya mtu mzima hovyo na bi nasma kidogo

  69. Mafuru masatu masangara on January 6th, 2008 4:41 pm

    Kazi nzuri sana hapo nawapongeza.Mmechanganya sana aina mbalimbali za miondoko ya muziki ni bora mngesort kulingana na aina ya music au geographical zone au hata inchi hii ingeleta ufanisi zaidi, lakini sasa kuna maharage, choroko, maini na matembele ndani ya chungu kimoja.Ni ushauri tu vinginevyo jitihada zenu zinaonekana.

  70. Malkiory - From Tampere(Finland) on January 6th, 2008 6:58 pm

    Najisikia nipo home uzingatia hapa Ughaibuni hatuna jinsi ya kuburudika na vitu adimu kama hivi. Hongera kwa Michuzi kwa kuturushia na zaidi kwa wana Jambo Net kwa kazi nzuri ya uandaaji. Cheers!

  71. Zumbe Togolay on January 6th, 2008 9:51 pm

    Hata huku kwa wenzetu Wahindi tumezipata za enzi za ‘Bumping’ Yenu Bar Kinondoni enzi hiizzoooooo!!!!!! Nawafagilia sana. Kazi nzuri

  72. Paul Nyingo on January 7th, 2008 5:10 am

    Nazidi kuwakubali hebujaribuni kuzitafuta na za mtu mmoja MTZ mwenzetu anaishi Japan anaitwa Fresh Jumbe Waziri Mkuu, zake za zamani zimetulia sana eg,mazingira yetu ,conjesta alipiga akiwa Nginde nk

  73. Alex on January 7th, 2008 8:59 am

    Asante sanaa kwa hizi nyimbo zilizopendwa —-shukrani kuzilete zote pamoja

  74. Boney on January 7th, 2008 12:04 pm

    Hakika kwa mtu wa enzi zetu anaguswa vilivyo na vibao hivi. Langu ni moja je utawezaje kusikiliza hizi nyimbo bila ya kusuasua? Sipati mtiririko mzuri zikipigwa zinakwama mara kwa mara, njia gani nitumie?

    Otherwise big-up kwa wana blog wote. Cheers.

  75. sasa on January 7th, 2008 3:35 pm

    Website nzuri collection ya muziki bomba sana ila please kuna wimbo uliimbwa na eddy shegi uitwao milima ya kwetu, kama utaupata na kuuweka kwenye list itakuwa zawadi kubwa mno.

  76. Monnie on January 7th, 2008 8:56 pm

    sina la kusema nasikia kulia tuu nikisikiliza hizi nyimbo pale zinaponikumbusha wakati wake,wapi na akina nani nilikuwa nao. wengine ni marehemu, wengine tumepotezana sijui wako wapi.Kwa kweli nawafagilia sana Jambo network kwa burudisho walilotuletea.Natamani kurudisha wakati nyuma lakini haiwezekani miaka ya 70 na 80 kwa kweli tulienjoy maisha .

  77. Sindbad on January 7th, 2008 9:17 pm

    Baab Kubwa, nafurahi sana kupata nyimbo za zamani hapa nakutakieni kila la kher na mafanikio .

    Ps
    Mickey Jones wa Copenhagen tafadhali chukua email adress hii ili tuwasiane kuna mambo mengi tuongee( jamalbaba@hotmail.com) tafadhali usidharau tunajuana

    Ahsanten wote

  78. Sindbad on January 7th, 2008 9:33 pm

    baab kubwa jambo

    mickey Jones tuwasiliane kwa email hii
    jamalbaba@hotmail.com
    muhimu sana tunajuana ila tumeachana muda mrefu

  79. MICKEY JONES on January 8th, 2008 7:29 pm

    Safari hii tumpe hongera Issa Michuzi kwa kuturudisha katika enzi hizoooo ambazo mziki ulienda pamoja na ushabiki wa mpira katika wakati wake wa ujana….sijuwi kama Sunday Manara,Chitete,Bonna Max,Adolf ukimtoa marehemu Mwijage na Kikwa watakubaliana na mimi….
    Jamalbaba nikumbushe kidogo ulikuwa kundi gani? mimi nilikuwa The Heroes na The Groove Makers na timu ya Taifa wote walikuwa washikaji….nikumbushe ndugu Jamal mickey@mail-online.dk au blog ya Issa Michuzi napiga hodi mlangoni kwake kila siku, nina mipango ya kumletea Michuzi rafiki yake “GERALD” wa LIVER-MAINI. kwa furaha ya kutupa burudani za kila siku toka bongo na ulimwengu wa nje…..Jamal burudika na zilipendwa unaikumbuka Geogina ya Marijani na Kasuku ya Afro 70?

  80. Maxence M. Melo on January 8th, 2008 8:45 pm

    Dah,

    Nawashukuruni nyote kwa kuweka maoni yenu juu ya kazi hizi tulizowawekea japo naona wengi wanamwambia mheshimiwa Michuzi aongeze nyimbo ama apunguze.

    UKWELI:

    Tutaendelea kuongeza nyimbo kadiri tunavyoweza na kuzitenganisha. Wale waloomba tuweke na taarab ni kuwa natarajia by next month naweza kuwa huru na kuzipandisha hapa.

    TAHADHARI:

    Epuka kuweka comment yako ikiwa imeambatana na barua pepe yako mfano kimeo@baabkubwa.com maana spams zitajazana kwenye inbox yako. Badala yake andika kimeo-AT-baabkubwa-DOT-com na unayempa barua pepe hiyo ataipata.

    MWISHO:
    Tunashukuru kwa ushirikiano wenu mimi pamoja na crew yangu. Tunasikitika kwa wale wanaolalamikia kuwa eti nyimbo hazichezi vema ama zinakoroma. Ni kuwa mtandao upande wenu uko na speed ya chini na njia mbadala ya kucheza miziki hiyo ni kuhakikisha computer yako kwanza ina Adobe Flash Player. Kama haina basi hautaweza kuipata miziki hii. Fanya kuvumilia kwa kubofya PAUSE ili miziki ijikite kwenye computer yako kwanza kisha anza kukandamiza mmoja baada ya mwingine.

    Nawatakia furaha katika mwaka 2008 na tuendelee kuwa pamoja. Hatupimi… Tangu 2004 na bado tunakuja tena kwa nguvu nyingine kubwa zaidi.

    Mac

  81. Maxence M. Melo on January 8th, 2008 8:49 pm

    Ooops!

    NYONGEZA:

    Kwa wale wenye mawazo ama ushauri msisite kutufahamisha. Kwa kuandika comments tu hatutaweza kuzisoma zote. Ujumbe ambao ungependa niushughulikie haraka sana ama kuufanyia kazi basi naomba utume via email kwa mac-AT-jambotanzania-DOT-net ama kwa namba ya simu tuma +255 713 444 649

    Karibu

  82. Ideka on January 8th, 2008 10:25 pm

    Kwa ujumla mimi nimefurahia sana, swali langu kubwa ni kwamba, ninaomba kununua hii collection yote, tafadhari sana naomba unijibu.
    anuani yangu ipo hapo juu.
    Kwa haraka zadi unaweza kunitumia tex katika number, {HIDDEN FOR SAFETY}.
    Asante,
    Ideka

  83. MICKEY JONES - COPENHAGEN DENMARK on January 8th, 2008 11:02 pm

    Mac ( Maxence)

    Tunashukuru kwa “dosier” yako kuhusu maendeleo ya hapo baadaye kwa wale wapenzi wa Taarab,kuhusu tatizo la nyimbo kutosikika vizuri,huku kwetu Scandinavien hatuna matatizo hayo,tunavipata vibao vyote vya enzi hizooo zetu za ujana bila wasi…..wape pole jamaa wenye mtandao uliyopitwa na wakati wake,maana wanakosa utamu wa kazi yenu…pia ilikuwa vizuri mlimsitua Michuzi, bwawa la maini mambo si mazuri kwa sasa amejiburudusha na zilipendwa kama sisi huku Scandinavien!!!

  84. Mfinanga, A on January 9th, 2008 10:04 am

    Keep up the good work my brother! nipozisikiliza hizo nyimbo, zinanipeleka mbali sana, haswa kwa sisi tulio mbali na nyumbani, natamani kuruka na ndege sasa hivi kurudi home. hayo ndiyo mambo wakati nikiwa Tambaza na Azania, kama tunaweza kurudisha miaka nyuma sijua ya mungu makubwa!!!!! great job guys keep it up.

  85. daudi mapande on January 9th, 2008 10:37 am

    jamani hii aza umeniumbua inanitoa machozi hasa niisikiapo sauti ya chiriku Hemed Maneti Ulaya na wakati huu awamu ya pili ikiwa imeshika hatamu.
    Mungu ailaze pema peponi roho ya Maneti na wengine wote waliotangulia mbele ya haki.

  86. steve on January 9th, 2008 2:46 pm

    nawafagilia wote walioanzisha blog hii yaani mnanikumbusha mbali sana najihisi kama nipo peponi vile mbarikiwe sana. mwaka mpya mwema nduguzanguni

  87. nanyanje on January 9th, 2008 3:07 pm

    Nyimbo ni safi kabisa na nina uhakika mtaongeza nyingi nyingi kama za hayati Franco Rwambo Makiadi, Msondo,Sikinde,Marquis Original, Masantula nk.
    Ila kilio ni kilekile cha wengi ukipiga zinakwamakwama kuimba mpaka uhondo wote unakwisha.

  88. masore on January 10th, 2008 8:27 am

    Mbona kimya hakuna zilipendwa wala vijana wa zamani

  89. Said Nanyanje on January 10th, 2008 3:43 pm

    Nyimbo ni safi kabisa na nina uhakika mtaongeza nyingi kama za hayati Franco Rwambo Makiadi, Msondo,Sikinde,Marquis Original, Masantula nk.
    Ila kilio ni kilekile cha wengi ukipiga zinakwamakwama kuimba mpaka uhondo wote unakwisha.

  90. slia on January 10th, 2008 8:31 pm

    whats a hell this songs are nice i like them. keep drives us crazy

  91. Chichi on January 11th, 2008 1:23 am

    Good job Guys! i admire your work Big Time!! Do you have any tracks from PAT SHANGE though? Would appreciate one or two of his great numbers!!
    Keep strong, cheers!
    :o)

  92. abdu on January 12th, 2008 4:58 pm

    Thank you mumenikumbusha mbali sana nyimbo ambazo huku ulaya ni Diamond japo ni za kale.tupeni nyingi hasa za bendi za dansi za KI BONGO ZAIDI.

  93. deo on January 12th, 2008 6:20 pm

    Wadau chukueni muda kusikilizeni website hina kila collection zote.chukua zaidi ya muda wa massa mane utashangaa, hata wale wanaosema kwamba hawawapati wapendwa wao , nikwamba take ur time this web is supere dupa.kilakitu kipo

  94. mimi on January 13th, 2008 2:11 am

    KWA KWELI MIE SIJUI NISEME NINI KAZI MLIYOFANYA NI KUBWA NYIMBO HIZI ZINANIKUMBUSHA MBALI SANA ENZI HIZO ZA GETI KALI HAPO KWA MZEE NANII HONGERA SANA NDUGU ZANGU

  95. Leonard on January 13th, 2008 3:47 am

    Okey, Nimeifurahia sana Taarabu ya mzee Bibi yetu Kidude “sikuachi leo na kesho peponi”, Mpe hai sana Bibi yetu hapo Nyumbani Dar. Nimeituma hii kama Dedication kwa Mke wangu Mpenzi aisikilize hapo home Dar-Tz kila jioni kabla hajalala. Za kale Zahabu Kweli bwana.

    Hi, kwa wote wanaofagilia zilizopendwa, nashauri kama mkiweza Msituchanganie nyimbo, tupeni za kibongo tu sisi wabongo ili tupate kufaidi nyumbani tu toka mwanzo mpaka mwisho kwani zinakumbusha sana Nyumbani, tunatamani sana kurudi nyumbani muda nao ndiyo hauendi haraka kabisa tumalize turudi kwetu Bongo tukae na familia zetu kwani tunahisi upweke sana kwetu na familia zetu kutukosa kwa muda mrefu.

    Leo- U.S.A

  96. Catunda on January 13th, 2008 5:59 pm

    Kazi nzuri sana kwacollection hiyo kwani ni kazi sana kupata miziki hiyo ya zamani na iliyokuwa ikipigwa kwa utaalam mkubwa ndio maana mpakaleo bado mizuri ..
    Ila kitu kimoja Programmer wenu inatakiwa awajue wanamuziki na nyimbo zao kwani nyimbo nyingi zimeandikwa artist tofauti na muziki wenyewe

    Catunda USA

  97. lulu jerry on January 14th, 2008 2:23 am

    Hej Yaani sijui niseme nini tu kwanza nakaribia miaka 40. lakini, kuna nyimbo zimeni touch saaana. kwani nilikuwa mtulivu wa maisha yangu lakini mpenda saana wa miziki na kutoka na marafiki zangu kudansi. Ila tu naona ule wimbo wa mama yake na Sofia mwimbaji siyo wa Tanzanite Band. Lakini kazi mliyoifanya ni Weldone 100%. Keep It Up.

  98. dennis on January 14th, 2008 10:16 am

    This is great, keep it up please.

    St Louis MO USA

  99. Robi on January 14th, 2008 11:42 am

    C mchezo inapendeza hasa kwa watu kama cc yaani wale vijana wa zamani, c utani nimezifurahia sana nyimbo hizi nyie vijana mwasema zilipendwa wengine bado mpaka leo twazipenda kaza buti

  100. Mochona on January 14th, 2008 8:56 pm

    Muziki Kabambe huu. Umenikumbusha mbali.

    Where can i get CDs of some of the tracks?
    I love to drive while the music is playing.

    Thanks in advance.

  101. ONE AFRICA DAIMA on January 15th, 2008 12:07 am

    How are you all African music lover, I am looking partner to hold the first African Music Award, the award is to recognize those who did amazing work, people like Franco Lwambo Makiadi etc. all African musician legends – What you think? Can we make happen? I am proud to African - ONE AFRICA DAIMA

  102. osima e on January 15th, 2008 11:27 pm

    kwa kweli nimefurahi sana kusikiliza hizi nyimbo za zamani hasa za msondo,ottu kwa ujumla nyimbo zote ni nzuri sana big up 2008 ni mimi mdau wa finland

  103. Yussuf Shoka Hamad on January 16th, 2008 3:59 am

    Hongera sana kwa blog hii.Kama kuna uwezekano naomba kununwa collection hii kama ilivyo.Ninaomba muongeze zaidi nyimbo za zamani na hata miaka ya tisiini ambazo hazivumi tena lakini zilikuwa kali nyakati hizo.

  104. Foya E on January 22nd, 2008 12:05 am

    kwa kusema kweli hii jambo network ni babu kubwa na inanikumbusha enzi za ujana wangu naitakia mafanikio blog hii idumu milele mmpenda vya nyumbani alie nchini Fnland nyumbani ni nyumbani bwana hata kuwe porini.

  105. Mfinanga, A on January 23rd, 2008 6:59 am

    Mambo ndiyo hayo ndugu yangu, sisi tulio mbali na nyumbani tulikuwa tuna sononeka, basi sasa tumefika nyumbani, haswa ule muziki wa Kasongo, unanifikisha wakati wa marehemu marijani na Les Trippers.

  106. kiburu on January 23rd, 2008 8:43 am

    Mimi binafsi nimeipenda sana hii mizike

  107. Robi on January 28th, 2008 3:45 pm

    Jamani 2naomba kuelekezwa kwa kupata hizi cd au dvd zenye nyimbo kama hizi manake huku uswahilini hakuna kazi yenu ni nzuri sana

  108. David- NC on January 29th, 2008 12:18 am

    Great Job, Keep it up!
    U know what! Im far away from home but, now I feel like im back home tz.
    Thank you so much!

  109. Yasser on February 2nd, 2008 1:09 am

    safi sana, miziki imetulia sana,ningefurahi zaidi kama ningeweza kusikiliza miziki ya hayati marijani Rajab.All in all, ipo makini yote kwa ujumla,ingawa kama ingekuwa ni non stop ingekuwa mwake zaidi.ila powa sana, respect you guys.. keep it real ~!

  110. Nerra on February 5th, 2008 8:13 am

    Muziki ni bombaaa! Big Up!

  111. Salha on February 6th, 2008 2:34 am

    I love this webbbbbbbbbbbbb
    Great job, keep it uppppppppppppppppppppppppppppppppp!!

  112. Brown Sheman on February 10th, 2008 11:50 pm

    habari ndo hii ragatse

  113. Lil' sis on February 11th, 2008 1:03 am

    OMG!!!! You guys are fabulous. Nilikua nasikiliza hizi nyimbo leo mara nasikia wimbo wa my big sister wa harusi…..Jamani 20th yrs anniversary ilikua Jan 18th…..NISHIKE MKONO - Kasongo Mpinda.

    Keep up the good work …Thanks so much

  114. basiga on February 13th, 2008 11:26 pm

    Kwa ufupi nawashukuru na kuwapongeza wataalam wanaohusika.
    site hii inanirudisha miaka ya 70 na 80.. sekondari, chuo, mnajua tena

  115. dotto on February 14th, 2008 3:53 pm

    umefanya mambo mazuri kwa kuweka zilipendwa, pia nakuomba utuwekee pia mziki wa mwambao hasa taarab sio mipasho. kama taarab nipepee, usiku wa fadhila,miadi kitu aziz, nnazama , waridi na nyingine nyingi.

  116. Mfinanga, A on February 16th, 2008 10:19 am

    Fantastic, this is great!!!!! guys , can you guys let us know where we can buy some of the music on this blog? great Zilipendwa kwa sisi tulio mbali na nyumabni.
    My E-mail is ayubissack@aol.com. shukrani taala bro!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

  117. WW MKOJERA - CHINA on February 16th, 2008 10:22 am

    Hongera kwa waandaaji na waongozaji wa site hii, nasifu kazi yenu kweli mbarikiwe. Najiona mwenye bahati kusikiliza site hii. Pongezi na Hongera kwa mchango wenu.

  118. CLAUS on February 19th, 2008 12:00 pm

    Nawapa shavu sana kwa jitihada zenu, Big up!!!

    Claus

  119. emmanuel edward on February 22nd, 2008 6:53 am

    Hongereni sana kwa kuthamini sana maendeleo na uhai wa mtanzania,
    Do not give up we are together untill we bring all corrupt figures in system to justice.

  120. lazaro maganga on February 22nd, 2008 9:10 pm

    Kumbe bongo tunaweza yani mnanikumbusha mbaliii miziki ni mizuri na kwa kwa kweli na collections yenu nimeipenda ila naomba mtutafutie oldnumbers za kizungu enzi hizo Bon em, abba group, cool n’ gang nk hapo mambo yatakuwa mazuri zaidi naomba maombi ya cc wadau wa hizi nazo myafanyie kazi pia naona maoni ya wadau wengine ni mazuri. BIG UP JF

    I LOVE TANZANIA

  121. PASCHAL PERFECTUS MASHAURI on February 23rd, 2008 10:53 am

    Dah kiukweli mambo ni mazuri kutokana na kwamba mnatupa vitu vile ambavyo tunavipenda na pia ukifuatilia maoni ya kila watu waliotangulia wana maoni mazuri sana ila cha muhimu muyafanie kazi maoni hayo BIG UP TO ALL PEOPLE TO WHOM THEY VIST TO THIS WEB…………………

  122. LJK on February 25th, 2008 1:36 am

    Naona hizi zilipendwa ni kali. Mbona mmesahau nyimbo za Mbaraka Mwinshehe, kama “Shida haina ngojangoja” na “Sembuli”. Tafadhali tuwekee hizi nyimbo sisi wapenzi wa Mbaraka Mwinshehe.

  123. Wangari on February 29th, 2008 11:40 pm

    Hello WebMaster:

    That stuff is off the Hizee! I really love your selections…

    W.

  124. mike on March 3rd, 2008 10:13 pm

    Mambo pooooa sana hasa abisina ,inanikumbusha sauti ya Nyiboma isiyochakaa.
    Twangojea playlist ingine kwa hamu.keep it up.

  125. agushe on March 7th, 2008 1:37 pm

    waziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, you make me hiiiiiiiiiiiiiii with this kind cool music kep it up guys we this relaxion ngoma here in kenya. po po.

  126. David on March 11th, 2008 9:01 am

    Kwa kweli nawapa BIG-UP kuturudisha miaka ya 47 ya uhuru wa tanzania wakati ule inaitwa Tanganyika.

    David Hizza

  127. adam mbura on March 26th, 2008 9:07 pm

    Kumbe bongo tunaweza, miziki inanikumbusha mbali sana.
    This wonderful!! Hongera.

  128. Wiki Mwanampuku on March 28th, 2008 2:14 pm

    Pongezi sana kwa site hii.Mnatukumbusha mbali,lakini mnatusaidia kuacha kusubiri vipindi vya Zilipendwa vya redio.Sasa mtu unasikiliza Zilipendwa pale utakapo.Haya ndio maendeleo.Keep it up and we are waiting for the new play list.For years I have been trying to find Bameli Soy by Tabu Ley.Now I have got it.
    THANKS AND KEEP IT UP

  129. Hassan siri on April 4th, 2008 8:54 am

    poa sana nimeipenda hii web.

  130. Mahmoud kiwala on April 17th, 2008 1:21 am

    Hongera sana kwa huduma zenu napenda munifahamishe jinsi ya kuzipa hususani kwenye cd pia naomba mungaliziweka nyimbo kwenye mpangilio wa bendi moja moja hata kama zitakuwa 5 au 10 baadaye nyengine zikaendelea mbele
    Ahsante

  131. Mikali Kinenekejo on April 23rd, 2008 10:24 am

    Aisee hivi niko ofisini boss akipita na mie nayarudi magoma japo niko nimekaa kwenye kiti mtu akitingishika au akitingisha mguu utamjua. akitingisha kifua, au mikono utajua tu kwamba mambo ni bam bam…. nyaisanga naye aaingie humu maana naye anatukuna sana na nyingi ambazo ziko hapa….. kwenyee kipindi chake..

    Thank you very much for puttimg up this.. it is wonderfu;l.
    Cheers and have a nice day.

  132. simon on April 23rd, 2008 11:50 am

    Big up! Jambo Network inapendeza kuona jitihada zenu keep it up!

  133. Kim Francis on April 25th, 2008 8:45 am

    Pongezi nzito(Mwajifya) kwenu Group yote ya JAMBO NETWORK -Zilipendwa.
    Nawatakieni kazi njema,mafanikio bora. Muwe watulivu, busara kupitia maoni yetu wasikilizaji na kuyafanyia kazi yale yanayofaa na yanawezekana kufanywa na Ofisi yenu. ZAIDI YA HAPOZILIPENDWA HOYEEEEEEEEEEEEEE

  134. Ridhiwani Ally on May 2nd, 2008 9:34 pm

    SOLUTE wazee,Hii ni soo watu wangu,ila wekeni na zile OldHiphop,zile za enzi zetu,itakuwa BAAAAABKUBWA ZAIDI,

  135. joshua on May 16th, 2008 7:23 pm

    Hizi zilipendwa zinakumbusha miaka ya themanini nikiwa bado mdogo nikiwa mtoto, ni safi sana hizi album.

  136. chilangu on May 16th, 2008 7:31 pm

    Endeleeeni na mambo mazuri kama haya ni poa kabisa ninapokuwa karibu na jambo hamna matata kama napata kile ninachotaka toka jambonet endeleeni kuleta mambo zaidi ya haya.

  137. MOSES on May 18th, 2008 10:13 pm

    wow. najisikia niko bongo. nikikaa na kusikiliza miziki ya kitanzania nikiwa hapa marekani. kuweni na moyo huo huo kuitangaza nchi.

    naomba maada . ninatafuta miziki ya kidini siipati .kama kuna web site . tafadhali naomba nitumieni.

    Mungu ibariki TAnzania

  138. kelvin on May 23rd, 2008 9:12 pm

    Inajitahidi kwa kusababisha kwa sababu ina2burudisha sana watz.

  139. NTIMI MTAWA on May 23rd, 2008 11:06 pm

    Ahh Jambo radio, mnaniburudisha vizuri, mnanipa vitu vya maana mno, hasa kibao cha PIGA UA TALAKA UTATOA, aaa mnankumbusha mbali, niko huku Bondeni lakini najiskia kama niko nyumbani licha ya XENOPHOBIA YAO, Ila Jambo inaniliwazisha, Jambo tuongezee vibao zaidi jama, hivitoshi, vibao kama NDOA NDOANO, VIJANA JAZZ ORCHESTRA WANA VITU VITAMU SANA VYA ZAMANI TAFADHARI JAMA JAMBO TULETEEE MAMBO. NAWASHUKURU SANA JAMBO MENDELEE NA KAZI NJEMA HIYO, MWENYEZI MUNGU AWABARIKI SANA. AFYA NJEMA JAMA.

  140. NTIMI MTAWA on May 23rd, 2008 11:09 pm

    Jambo jambo jambo radio jama si mchezo hakuna kulala we kama ni mpenzi wa muziki wa enzi hizo usisite nenda jambo radio network, wanakupa mambo, jama

  141. NTIMI MTAWA on May 23rd, 2008 11:27 pm

    jamani Jambo kuna Bendi ilikuwa inaitwa TANCAT ALMAS ORCHESTRA hamna vibao vyao, Bandi kama NGORONGORO HEROS nyimbo kama KAMBWEMBWE,POKEA SALAMU, BENDI KAMA RUAHA JAZZ BANDI, JAMA HEBU JITAHIDI MTULETEE VITU HIVYO , ni jambo radio pekee inaweza kutuletea mambo kama hayo. Mungu ibariki Africa , Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki JAMBO RADIO kwa kai you nzuri.

  142. Ben on June 5th, 2008 10:53 am

    Great stuff!

    But why cant you guys let us download these gims and enjoy them in our ipods???

  143. david musika on June 9th, 2008 6:37 am

    Tafadhali naomba kujuwa wapi naweza kupata hizi nyimbo zote hizi za kale, kwani zinanikumbusha mambo mengi, Tafadhali nazihitaji!!!! najihisi 2008 kama enzi zile zangu, kwani si muda wote nakaa kwenye computer na kuweza kusikiliza, napenda kusikiliza kila niendako, offisini, kwenye gari hata popote pale-sikinde,otu, remy,tabuley,Hata mwanyama wa msituni wanapenda twist-watoto wangu wanoupenda sana

  144. majuva amina on June 16th, 2008 10:28 pm

    Hongereni sana kwa kutuchombezea nyimbo nzuri . Tunajisikia tupo home japo tupo ughaibuni. KEEP IT UP.

  145. Salha Bin Mende on June 17th, 2008 1:26 pm

    Question naweza kupata wapi nyimbo hizi? Ninagraduate June 28, 2008 zimebakia week mbili naweza kupata wapi nyimbo hizi. Kama kuna website amboyo naweza kuangiza nyimbo hizi. please nijulisheni

    Proud to be TANZANIA

  146. Ansbert Ngurumo on June 24th, 2008 11:36 pm

    Asanteni kwa burudani. Shukrani za ziada zimwendee rafiki yangu Ben Kimbache wa London, aliyenijulisha tovuti hii. Niko mbali na nyumbani, lakini muziki huu unanifanya nijihisi niko nyumbani Tanzania. Ni muziki murua, uliopangiliwa vema, unaonikumbusha mbali - enzi zile. Ana kweli zilipendwa, zinapendwa!

  147. Chicago on June 27th, 2008 6:55 am

    Hongereni sana kwa kutukumbusha nyimbo nzuri za zamani. Naweza kupata wapi nyimbo hizi. Hapa Dar-es-salaam

  148. Riyami on June 28th, 2008 11:24 am

    Hapa ukweli mlikaa nakufikiri nini chakuwafurahisha wateja,,kikao chenu kimefanikiwa namafanikio mmeyaona sina mengi yakusema ila natoa shukrani za dhati kutukumbusha wapi tulikua kwa miziki tunayopata furaha ilioje! ahsanteni sana.

  149. Albert Manga on July 19th, 2008 5:55 pm

    What an entertainment you are rendering!! you all deserve a big up. is it possible to get some wonderful musics? I can not conclude a day without citing this web/ blog if you like.

  150. Cosmas Mwazo on July 25th, 2008 12:52 pm

    Nashukuru sana kwa juhudi zenu kututumbuiza sisi wa zama. Ningeomba mtupe vibao vya orchestre Kiam, shamashama, kamale,veve na wengineo

  151. Irene on July 25th, 2008 3:16 pm

    Yaani hizi nyimbo ni bomba has in working areas we are refreshed alot,naomba mtuwekee akudo,twanga na FM academia za kumwaga.Nawatakia mafanikio mema mko creative sana

  152. Sindbad on July 26th, 2008 11:32 pm

    kweli mambo makubwa sana humu lakini mradi salama .

  153. vincent on July 29th, 2008 1:55 am

    Hi there,
    I want to congratulate whoever set this up.
    Men I am enjoying this to the maximum.
    keep up the good work.

  154. Zakhia Rajab Soka on July 30th, 2008 1:47 pm

    Kweli mmefanya kazi nzuri sana……..endeleeni kuongeza zilipendwa nyingi zaidi.
    mnakubalika

  155. moshiro jacob on August 16th, 2008 1:22 am

    nawapongeza sana kwa kutuwekea nyimbo hizi za zamani kwenye web site.
    ombi langu lipo kwenye jinsi ya kuzidownload na kuzihifadhi kwenye PC ili niweze kuzisikiliza wakati sipo online.
    So kama kuna uwezekano naomba mnielekeze.

  156. Bakari Fumbwe on August 19th, 2008 10:01 am

    Kwa kweli nimewafurahia kwa burudani nzuri ya zilipendwa mjitahidi mtuboreshee na zilipendwa za taarab ziwepo nyingi kama za bolingo na nyinginezo

  157. Joe Das on August 24th, 2008 3:29 pm

    Naomba vibao vya bendi ya tancat arumas navyo mviweke maana jambo redio pekee ndiyo mnao konga nyoyo zetu nawafagilia kwa kazi nzuri

  158. Joe Das on August 24th, 2008 3:32 pm

    samahani nimekosea ni tancat almas

  159. Jimmy J. on August 30th, 2008 3:24 pm

    Hapa ndipo ninapotumia siku yangu ya mapumziko,Hongereni kwa kazi nzuri.

  160. isack kessi on September 10th, 2008 1:56 pm

    hii ni top notch jambo radio, ila ombi ni moja kama mkiweza kuongeza nyimbo nyingine nyingi hatutasema no;
    pamoja na kulala na kufanya mazoezi kusikiliza hii radio kuanapunguza stress so keep ip up guyz

  161. florens ottaru on September 12th, 2008 9:25 am

    nimefurahia sana kunikumbushia enzi zetu mkuu sio siri kuna nyimbo moja hapa inanitoa machozi all we need africa.

  162. florens ottaru on September 12th, 2008 9:28 am

    tuna mengi ya kuifanyia africa hasa nyumban tanzania. from bangkok thai

  163. florens ottaru on September 12th, 2008 9:36 am

    samahani ningeomba kama ningeweza kuzipata hizi nyimbo kama zilivyo ndugu yangu.

  164. Daywell on September 18th, 2008 6:22 pm

    zitatakuja zitaondoka nyie ni mwisho,wakumbushe watu kuwa ya kale dhahabu

  165. JOHN.KASHAIJA on September 21st, 2008 1:57 am

    THANKS ALL BOGOS 4 ZILIPENDWA.MIMI NIKO HAPA. RAIA WA CANADA.
    BUT NYIMBO ZIMENIRUDISHA .MWAKA 1977 AT IHUNGO SEC.BUKOBA
    TANZANIA.TUKIJIMWAGA NA TOTOS ZA RUGAMBWA. GOD BLESS ALL.

  166. NTIMI MTAWA on September 27th, 2008 1:26 am

    kuna huyu bwana anaitwa MSHASHO the DOGG kutoka Namibia alikuwa kwenye Channel O award kama mna tracks zake tafadhari naomba mzipachike mahali ili wapenzi tuburudike.

  167. Godfrey Alban Kayumbo on October 4th, 2008 9:24 pm

    Tunashukuru sana kwa nyimbo hizi kwani zina ujumbe muhimu sana katika maisha yetu haya,pia zina tukumbusha muziki wa kiafrika hasa Afrika ya mashariki kipindi/enzi za baba zetu.

    Hongereni kwa kazi nzuri,Godfrey Alban,Western Cape,RSA.

  168. Jayfour Rama on October 5th, 2008 4:07 pm

    Big up webmaster.

    The idea of having this old music site for old and middle age like me is extremely good, keep it up.

    But it will be ideal to tell us where to get a copy of these golden old songs, this is b’se sometimes when network is down you won’t enjoy as aimed.

    So like others said, help us by informing where physically we can get a copy of these nice collections.

    Thank you very much for being creative and socially.

  169. hans on October 6th, 2008 4:40 am

    nimeshindwa kuvumilia jamani, nimejikuta machozi yananitoka, nimekumuka mbali sana jamani, aah wee acha tu.
    Nimekumbuka maisha ya miaka 80 tukiwa tumezungukwa na umaskini ambao siwezi kuusahau na nyimbo kama hizi tunazisikiliza kwa majirani maana hata radio hatukuwa nayo

  170. kip bwana ya cheptoo on October 7th, 2008 2:56 pm

    i loooove this website

Got something to say?